Sunday, June 5, 2016

KUTANA NA BINTI ANAYETUMIA LAPTOP NA SIMU KWA ULIMI

Dhana ya mtu kuwa na ulemavu katika maisha ndiyo kigezo cha kumfanya ashindwe kushughulika na jambo lolote sio sahihi kabisa, kama ambavyo imekuwa ikithibitishwa na watu wenye changamoto za ulemavu wa viungo kwa kufanya mambo makubwa na kuendelea kufurahia wanachokifanya.

Ukiacha changamoto ambazo zinawakabili watu hao, lakini bado wemeendelea kuwa mifano kwa watu wengine kama ilivyo kila binadamu ana historia yake ambayo inaweza kumvutia mtu na kumfanya ajifunze mambo mengi ambayo anaweza kuyatumia kama fursa katika maisha ya kila siku.

 Nursamawati Mahmud3

Nursamawati Mahmud ni msichana mwenye asili ya India ambaye anakumbwa na changamoto za kimaumbile kwa kuwa na ulemavu wa miguu na mikono na kumfanya alazimike kutumia ulimi wake pekee katika fanya mambo yake hususani matumizi ya LapTop na simu za mikononi.

 Nursamawati Mahmud1

No comments:

Post a Comment

Comment here