Sunday, June 5, 2016

YALIYOJILI KATIKA BASH LA MMU

tarehe 4 ya mwezi wa saba,wanafunzi wa mwaka wa tatu MMU wanatarajiwa kuanza kufanya mitihani ya mwisho ambapo mwezi wa 11 ndiyo watahitimu rasmi.Lakini katika kuonyesha upendo na umoja waliamua kuandaa sherehe (BAASH) ili kuagana na wanajumuia wengine wa MMU.


Sherehe hiyo ilianza majira ya jioni ya jana saa 11,ambapo wahudhuriaji walipata fursa ya kusikiliza semina ya mfuko wa hifadhi ya jamii ya PSPF na baadae takribani wanafunzi wote walisajiliwa katika mfuko huo BURE kabisa ikiwa na pamoja na kupiga picha na ujazwaji wa fomu.viongozi na watu waliotoa mchango katika shughuli za MMUSO walitunukiwa vyeti na medali,baadhi ya watu hao ni lembrus mchome,baraka chitalilo,mboyi mkirya na n.k


Baada ya semina hiyo,majira ya saa 1 usiku,wahudhuriaji walipata chakula ili kujiandaa kwenda katika "session" ya usiku,huko sasa PALINOGAJE? unajua kilitokea nini?wacha nikujuze.Watu walipendeza sana kiukweli wake kwa waume asikwambie mtu.Kila mtu alijitahidi kuvunja kabati lake lake,kulikuwa na kosta mbili kwa ajili ya kuwapeleka mpaka eneo la tukio.

Wakati tupo kwenye moja ya kosta anbayo alipanda mwenyekiti wa sharehe hizo ndugu mboyi mkirya ,alifanya kama utani kwa kuwaambia watu mambo mbalimbali na moja jambo hilo ni kuacha kumuabisha kwa kutapika dagaa.

Mungu si baraka chitalilo,tulifika salama na pati ilianza kwa burudani ya mziki maridadi kutoka kwa dj maridaidi katika ukumbi huo.

MAMBO YA KUSIKITISHA KATIKA BAASH
  • mboyi mkarya alipata matatizo ya kutapika
  • neema swai alidondoka ukumbini
  • na kuna mwanafunzi anafahamika kwa jina la kaunda,alimeza simu(hazijathibitishwa)
                                   #AHSANTE KWA KUISOMA

No comments:

Post a Comment

Comment here