MWANZA: MTOTO MWENYE UMRI WA SIKU 1 AIBWA HOSPITALINI
Mtoto wa siku moja ameibwa katika
mazingira ya kutatanisha katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando, akiwa
pembeni mwa mama yake aliyekuwa amelala, mwenye umri wa miaka 16.
Akizungumzia uporaji huo jana, Kamanda
wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Justus Kamugisha, amesema aliyepora mtoto
huyo aliingia ndani ya wodi ya wazazi ya Hospitali ya Rufaa ya Bugando,
akiwa amejifunga ushungi.
“Alipoingia
wodini alikuta mama wa mtoto amesinzia akiwa peke yake wodini, ndipo
akamuiba mtoto wake wa kike mwenye umri wa siku moja na kuondoka naye
kwenda kusikojulikana,” alisema.
Kwa mujibu wa Kamanda Kamugisha, Jeshi
la Polisi limeanza uchunguzi wa tukio hilo kwa kuhoji wauguzi, walinzi
na wazazi waliokuwa wamelazwa wodini hapo.
Katika hatua nyingine, Kamanda Kamugisha
amesema Jeshi la Polisi mkoani humo, litaanza kufanya uhakiki wa silaha
kuanzia Aprili mosi hadi Juni 30 mwaka huu, katika ofisi za makamanda
wa Polisi wa wilaya zote za Mkoa wa Mwanza.
No comments:
Post a Comment
Comment here