Saturday, April 23, 2016

UKWELI KUHUSU PENZI JIPYA LA SHILOLE NA MSANII HUYU WA BONGO FLEVANI

Post za Hitmaker wa Nyang’ang’a Zuwema Mohamed maarufu kama Shilole na mwanamuziki chipukizi Nedy Music ambaye yupo chini ya usimamizi mahiri wa meneja Mubenga, zimewafanya wadau wa muziki kuhisi kuwa huenda kuna mahusiano kati yao.

MUBENGA NA KIBABUDE (2) Baada ya jitihada za kuwatafuta Nedy Music na Shilole kugonga mwamba, mtembezi iliamua kupiga story na meneja wa msanii Nedy Music, Mubenga ambaye ameeleza kuwa anazisikia taarifa hizo kama watu wengine wanavyozisikia

“Nimezisikia taarifa hizo kama watu wengine lakini nilipo jaribu kumuuliza Nedy Music amekanusha kuwepo kwa mahusiano yake na Shilole, ila naimani hawezi kunificha kitu” Alisema Mubenga.

Mubenga ameongeza kuwa hata kama ikitokea Nedy Music akaja kutoka kimapenzi na Shilole hawezi kumkataza kwani umri wake unaruhusu, ila mahusiano hayo yakiathiri kazi yake ataingilia kati kwani kazi yake ni kufanikisha msanii wake anafanya vizuri.

No comments:

Post a Comment

Comment here