Tuesday, May 17, 2016

HAMSINI KIKWAZO MABASI YA MWENDO KASI

Huduma ya Mabasi ya Mwendo Kasi imeanza rasmi jana kwa abiria kulipa nauli elekezi huku ikikumbwa na changamoto kadhaa ambazo zimesababisha kuwepo malalamiko kutoka kwa abiria lakini uongozi wa mabasi hayo umesema unayafanyia kazi ili kupata ufumbuzi wa kudumu.

Wakizungumza  baadhi ya abiria wametoa malalamiko yao wakidai kuwa wamefika kwenye kituo cha Ubungo muda mrefu ila tatizo walilokumbana nalo ni kukosekana kwa chenchi ambapo wanaokatisha tiketi wanadai chenchi ya hamsini ni ngumu kupatikana kutokana na abiria kuwa wengi hivyo inawalazimu kuwataka abiria kuwa wavumilivu ili waweze kuwatafutia.

 

Deus Mgawa ni Meneja Mahusiano wa UDART amekiri kuwepo kwa changamoto hizo huku akidai kuwa watazifanyia kazi kwa haraka ikiwemo kuharakisha kwa mfumo wa utumiaji kadi mfumo ambao utasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza foleni ya abiria katika ukataji wa tiketi.

 

No comments:

Post a Comment

Comment here