MADRID DERBY KUTIKISA JIJI LA MILAN LEO
Ni fainali ya michuano yenye msisimko
mkubwa ya UEFA Champions League ambayo leo inafika tamati, vidume wawili
kutoka nchi na jiji moja la Madrid yaani Real Madrid ya Zidane pamoja
na Atletico Madrid ya Simeone nani kuchukua kombe hilo kwa mara ya
kwanza? wewe unaishabikia timu ipi?
HISTORIA
Michuano hii ina umri wa mtu tena kwa
aliyezaliwa miaka ya 1990’s inawezekana wakaiita babu michuano hii, ina
miaka 61 yaani imeanzishwa rasmi 1955 kumbuka wazo la michuano hii
limetoka kwa Santiago Bernabeu Yeste mwaka uliotajwa hapo juu yeye
alianzisha michuano inayoitwa L’Equipe au Copa Latina, timu zilizokuwa
zinashiriki kutoka Ufaransa, Italia, Ureno na Hispania ambapo baadaye
ikabadilishwa jina na kuyaita UEFA CUP, miongoni mwa timu za awali
kuchukua kombe hili ni Real Madrid, Benfica na Ac Milan.
BINGWA WA KIHISTORIA
Real Madrid ndiyo haswa bingwa mara
nyingi wa michuano hii na ndio timu ya awali kuchukua kombe hili na
amelichukua mara tano mfululizo wakati huo linaitwa UEFA Cup 1955 hadi
1960 kwa ujumla Madrid kachukua mara 10, kumbuka kuwa tangu lifanyiwe
marekebisho 1992 hakuna timu iliyochukua mara mbili mfululizo.
ZINEDINE NA SIMEONE
Wote walikuwa wachezaji kipindi hicho na
walicheza timu hizo wanazofundisha sasa na wamekuwa makocha wa timu
hizo. Yoyote atakayechukua ataweka historia kwa kuchukua mara ya kwanza
kwa upande wa makocha wakati kwa timu zenyewe Real Madrid wamechukua
mara 10 wanasubiria historia ya kuchukua mara 11 wakati Atletico kama
wakichukua itakuwa mara ya kwanza.
No comments:
Post a Comment
Comment here