Tuesday, May 31, 2016

TAARIFA MPYA ZA MGOMO CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM (UDSM)

Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wamegoma wakishinikiza Bodi ya Mikopo kutoa fedha kwa ajili ya kujikimu.

 

Makamu wa Rais wa Serikali ya Wanafunzi chuoni hapo, Shamila Mshengema amesema mgomo huo ni matokeo ya taarifa zisizoeleweka zilizokuwa zikitolewa na Bodi ya Mikopo (HELSB) juu ya lini fedha hizo zitatolewa.

Kama ilivyo ada fedha hizo za kujikimu huingizwa kwenye akaunti za wanafunzi kila baada ya siku 60, lakini mpaka sasa wanafunzi hao wanadai kuwa zimetimia wiki pasipo kuwekewa chochote kwenye akaunti zao.

Mgomo huo unakuja zikiwa zimesalia siku mbili Rais Magufuli kuzuru chuo hicho kwa ajili uzinduzi wa Maktaba.

HUU NDIYO UKWELI KUHUSU MGOMO WA UDOM 

UPINZANI HAUNA IMANI NA NAIBU SPIKA KWA JAMBO HILI 

No comments:

Post a Comment

Comment here