Thursday, May 19, 2016

USHOGA UNAZIDI KUENEA DUNIANI

Rais wa Mexico Enrique Pena Nieto, ametoa pendekezo la kuhalalisha ‘ushoga’ na ndoa za jinsia moja nchini.

Akihutubia kwenye hafla ya maadhimisho ya siku ya kupinga ubaguzi ulimwenguni, Pena Nieto alisema kwamba yupo tayari kutia saini kanuni ya kuhalalisha ndoa za jinsia moja nchini humo.

Rais huyo pia alifahamisha kuandaa kampeni maalum ya kutetea haki za wapenzi wa jinsia moja na kufanyia marekebisho katiba kwa ajili ya suala hilo.

Kwa mujibu wa pendekezo la rais, kipengele cha 4 cha katiba ya taifa ndicho kinacholengwa kubadilishwa ili kuleta haki na uhuru wa ndoa za aina yote bila ya ubaguzi.

No comments:

Post a Comment

Comment here