Friday, May 20, 2016

WABUNGE UKAWA NUSURA WAMPIGE MBUNGE WA CCM

Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Jackline Msongozi hivi karibuni amenusurika kipigo kutoka kwa wabunge wanawake wa UKAWA baada ya kuwaeleza kuwa upande huo una wabunge wawili tu wenye michango ya maana ambao ni Upendo Peneza (Viti Maalumu Chadema) na Magdalena Sakaya (CUF).

[​IMG]

Akichangia mjadala wa Bajeti kwa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Msongozi aliishambulia Kambi ya Upinzani akieleza kuwa kuna mlevi mmoja amechangia upande wa upinzani kuhusu uuzwaji wa nyumba za Serikali wakati waliohusika na uuzwaji huo wamehamia upinzani ambao ni Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye.

Mara baada ya Bunge kuahirishwa wabunge wanawake wa upinzani wakiongozwa na Sabrina Sungura na Ester Matiko walimfuata Msongozi wakitaka kumshambulia, lakini aliondoka moja kwa moja pasipo kusimama popote.

Sungura alipoulizwa alisema kuwa mbunge huyo angesimama wangemshughulikia.

No comments:

Post a Comment

Comment here