Sunday, May 8, 2016

YANGA NA TUMBUA TUMBUA KAMA MAGUFULI

Mchezo wa kuwania kufuzu hatua ya makundi michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika mkondo wa kwanza kati ya Yanga na Sagrado Esparanca ya Angola umemalizika kwenye uwanja wa taifa na Yanga imeibuka na ushindi wa mabao mawili kwa sifuri.

 Young Africans SC (logo).png

Mabadiliko yaliyofanywa na benchi la ufundi la Yanga katika kipindi cha pili kuwatoa Malimi Busungu na Salum Telela na nafasi zao kuchukuliwa na Geofrey Mwashiuya na Mbuyu Twite yameisaidia timu hiyo kutoka mitaa ya Jangwani Kariakoo kuibuka na ushindi.

Dakika ya 71 Msuva alifungua ukurasa wa ushindi kwa kupachika bao la kwanza baada ya kupokea krosi kutoka kwa  Mwashiuya. Mchezo uliendelea kwa Yanga kushambulia lango la Sagrado hadi dakika za nyongeza ambapo Matheo Antony alipiga shuti la kushitukiza lililowababatiza walinzi wa Sagrado na kuingia nyavuni.

Filimbi ya mwisho ya mwamuzi kutoka Ghana ili iruhusu Yanga kuondoka na ushindi wa mabao hayo 2 – 0. Kwa ushindi huo Yanga imejiweka kwenye mazingira mazuri ya kusonga mbele kwenye michuano hii kwani itahitaji sare tu au isifungwe zaidi ya bao 1 kwenye mchezo wa marudio nchini Angola.

No comments:

Post a Comment

Comment here