Monday, June 13, 2016

ABDU KIBA KUTUA WCB?

“Nipo tayari naangalia pesa, kama pesa zitakuwepo na wakihitaji kufanya kazi na mimi naweza nikafanya kazi chini ya lebo hiyo,”.

13266823_882952098517543_720315630_n

Kama umekuwa ukichanganywa na hicho alichokiongea  Abdu Kiba kuwa yupo tayari kusaini mkataba wa kufanya kazi na lebo ya WCB inayomilikiwa na Diamond kama hela itawekwa mezani, basi usichanganyikiwe taarifa hizo ni za kweli na Abdu Kiba amethibitisha kuwa aliyaongea hayo alipokuwa akifanyiwa mahojiano kwenye kipindi cha Planet Bongo.

Baada ya utata maneno hayo Abdu Kiba amelazimika kuvunja ukimya kwa kusema kuwa mashabiki wamelipokea vibaya na kwamba hakumaanisha kama hivyo lilivyopokelewa watu.

SWALI LA MSINGI: Kama watu wamelipokea vibaya wewe ulimaanisha nini? yote ameyajibu kwenye sauti hapo chini na kusisitiza kuwa hana mpango wa kuihama menejimenti yake kwa sasa.

No comments:

Post a Comment

Comment here