Kampuni kubwa ya
teknolojia ya Apple imesema mauzo ya simu zake zijulikanazo kama iPhone
yameanza kupungua na kwamba mauzo hayo yanatarajiwa kushuka kwa mara ya
kwanza tangu kuzinduliwa kwa simu hizo 2007.
Kampuni hiyo kutoka
Marekani iliuza simu 74.8 milioni robo ya kwanza ya mwaka huu wa kifedha
ikilinganishwa na simu 74.5 milioni robo ya kwanza ya mwaka
uliotangulia. Apple imesema mauzo kutoka kwa robo ijayo yanatarajiwa
kuwa kati ya $50 bilioni na $53 bilioni, kiasi ambacho kitakuwa chini ya
mauzo ya $58 bilioni kipindi sawa mwaka uliotangulia.Hii itakuwa mara ya kwanza kwa mauzo ya iPhone kushuka tangu kuzinduliwa kwa simu hizo za kisasa.
Mauzo ya iPhone yalichangia asilimia 68 ya faina ya kampuni ya Apple mwaka jana.
Kushuka kwa mauzo ya kampuni hiyo kunadaiwa kutokana na kiwango cha uchumi wa China kushuka.
Mauzo ya Apple nchini China, Hong Kong na Taiwan yaliongezeka 14%, lakini kiwango hicho cha ukuaji ni cha chini mno kikilinganishwa na ukuaji wa 70% ulioshuhudiwa mwaka mmoja uliopita.
No comments:
Post a Comment
Comment here