ADHABU NYINGINE KALI KUTOKA KWA JPM
Baada ya jamii ya wakazi wa Kata ya
Karansi, Wilaya ya Siha Mkoani Kilimanjaro kukubaliana kuwa wanawake
watakaovaa sketi fupi na vijana watakaovalia suruali chini ya kiuno
kuadhibiwa kwa kuchapwa viboko 60 hadi 70, kali nyingine imeibuka baada
ya Rais Magufuli kutembelea Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakati akiweka
jiwe la msingi la ujenzi wa Maktaba ya kisasa chuoni hapo.
Rais
Magufuli ametoa kali nyingine baada ya kusema wanaopita kwenye barabara
za mwendokasi zichomolewe tairi za magari yao kisha ziuzwe baada ya
kupelekwa kituoni ili waharibifu wa barabara hizo nao wapate hasara kwa
kuwa serikali iliingia gharama kubwa ya sh. bilioni 388 katika ujenzi wa
miundombinu wa Mradi wa Mabasi ya Mwendokasi.
“Mtu
anapeleka gari lake humo anaondoka kule anazunguka humu wakati kuna
barabara nyingine ipo kwa ajili yake, ‘no body is taking action’ …
anatoka kule anampita traffic wala hamshiki na kwenda kulizuia gari lake
likakae polisi, halafu siku akija kulichukua liwe halina matairi
hatapita tena kwenye barabara ambayo hatakiwi, na akiuliza mbona halina
matairi unamwambia lilikuja hivi hivi” alisisitiza Dk. Magufuli.
Hivi
karibuni Rais Magufuli alitoa kali nyingine baada ya kusema
wafanyabiashara wote wanaoihujumu serikali yake kwa kuficha sukari ili
wajineemeshe hata wafumbia macho, akasema “Nataka niwaambie sukari huwezi kuificha kama sindano, wafanyabiashara wote ambao wameficha sukari wale ni wahujumu uchumi; tutachukuwa sukari hiyo na tutaigawa bure na hawatafanya biashara maishani hapa Tanzania“.
No comments:
Post a Comment
Comment here