Friday, June 3, 2016
MATARAJIO YA KUSAINI PESA YA KUJIKIMU KWA WANACHUO YANAKUJA
kumekuwa na hali ya sintofahamu kuhusiana na pesa ya kujikimu wanachuo (boom) katika vyuo mbalimbali ambapo pesa hiyo hutolewa kila baada ya siku 60,na kwa mujibu wa kalenda ya bodi ya mikopo siku 60 zao zinaishia kesho.
Akiongea na adamukihomile.com,waziri mkuu wa serikali ya wanafunzi wa MMU amesema kuwa,matarajio yao siku ya kesho pesa za wanachuo hapa MMU zitawekwa katika akaunti kwa ajili ya kupewa wanafunzi pesa zao.
Aidha aliongeza kuwa na kama hazitawekwa kesho,basi itakuwa tarehe 11 kwani pia bodi ya mikopo ina tabia kuwahi au kuchelewa kwa siku 7,hivyo basi kuhusu kusaini wanachuo zao,itategemea na ni siku ipi pesa itaingizwa kwenye akaunti,kama itawekwa tarehe 4 yaani kesho,basi wanachuo watasaini jumatatu ya tarehe 6 na kama itawekwa tarehe 11,pesa itasainiwa na wanachuo tarehe 13.
pia waziri amewakumbusha wanachuo wa MMU kuwa tarehe 17-20 ,maofisa wa bodi ya mikopo watakuwepo chuoni hapo na kila mwanafunzi anapaswa kuwepo katika zoezi hilo akiwa na kitambulisho cha chuo na "passbook yake ".
#AHSANTE KWA KUISOMA
.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment
Comment here