Sunday, June 5, 2016

HAWA NDIO MABEKI 10 VITASA KWENYE MICHUANO YA EURO2016


Moja ya nafasi muhimu uwanjani ni sehemu ya ulinzi. Hii ni muhimu kwa timu yoyote ya mpira wa miguu ili iweze kupata ushindi ni lazima ukuta wao uhakikishe unazuia mashambulizi ya timu pinzani.

Kuelekea michuano ya EURO2016 nchini Ufaransa leo tupate wasaa wa kutazama mabeki kumi bora wanaotarajiwa kufanya makubwa na kuzisaidia timu zao za taifa.

10. Jose Fonte: Huyu ni mlinzi wa kati raia wa Ureno mwenye umri wa miaka 32 na amekuwa na msimu mzuri ndani ya Southampton hivyo atakuwa kwenye ukuta wa Ureno akiwasaidia Louis Nani na Ronaldo kuhakikisha wanashinda.

11. Stephan Lichtseiner: Ni beki wa kulia wa Juventus na Timu ya Taifa ya Uswisi. Naye atakuwepo kuhakikisha nchi yake inaondoka na ubingwa wa Ulaya.

12. Sime Vrsaljiko: Ni mlinzi wa kati wa Klabu ya Napoli na Timu ya Taifa ya Croatia. Atakuwa anawakilisha taifa lake na Ivan Rakitic pamoja na Luka Modric.

13. Toby Alderweireld: Raia wa Ubeligiji na beki wa kati wa Tottenham. Amechukua nafasi ya Vincent Kopany hivyo atakuwa akina Eden Hazard na Kevin De Bruyne kuhakikisha kombe linaenda kwao.

14.Elseid Hysaj: Ni raia wa Albania anayekipiga Napoli kama mlinzi wa kati naye ni moja ya nyota wanaotarajiwa kufanya vizuri EURO2016.

15. Juanfran: Nyota wa Hispania na Atletico Madrid naye yumo katika walinzi kumi wanaotajiwa kufanya vizuri. Anakumbukwa kwa kukosa penati kwenye mchezo wa fainali ya Uefa dhidi Real Madrid na kuikosesha ubingwa timu yake.

16. Mats Hummels: Ilikuwa roho ya Dortmund lakini tayari imenyakuliwa na Bayern Munich kwa ajili ya msimu ujao. Atakuwa anaongoza ukuta wa Ujerumani kuhakikisha wanatwaa ubingwa huo.

17. David Alaba: Ni kipenzi cha Pep Guardiola akiwa na uwezo wa kucheza kama kiungo ama winga, japo hucheza sana kama mlinzi wa kushoto. Atakuwa na kikosi cha Austria wakisaka taji la EURO2016.

18. Sergio Ramos: Ni mlinzi wa kisasa anayejua kufunga pale inapobidi afanye vile na hapo ndipo anakumbukwa vizuri kwa kufunga kwenye fainali mbili za Uefa zote dhidi ya Atletico Madrid. Atakuwa na kikosi cha Hispania wakisaka taji la Euro kwa mara ya nne.

19. Leonardo Bonucci: Raia wa Italia anafahamika kama mtaalam wa ‘Tackles’. Anakipiga Juventus na atakuwa na timu yake ya Italia nchini Ufaransa wakipambana kusaka ubingwa wa EURO2016.

Hao ndio walinzi wanaotarajiwa kuzitetea timu zao kwenye michuano inayoanza June10 nchini Ufaransa.

No comments:

Post a Comment

Comment here