MAREKANI KUIPATIA TANZANIA DOLA MILIONI 800

Uthibitisho wa kutolewa kwa msaada huo,
umetangazwa na Balozi wa Marekani nchini, Mark Childress aliyekutana na
kufanya mazungumzo na Rais John Magufuli katika Ikulu ya Dar es Salaam
jana.
Balozi Childress alisema kutolewa kwa
fedha hizo ni uthibitisho kuwa kutotolewa kwa fedha za awamu ya pili ya
Mradi wa Changamoto za Milenia (MCC-2), hakujaondoa uhusiano na
ushirikiano wa Tanzania na Marekani, ikiwemo utoaji wa misaada ya
maendeleo.
“Tumezungumza mambo kadhaa, na wiki hii
Tanzania na Marekani kupitia shirika letu la misaada la USAID
tunatarajia kutiliana saini mkataba wa zaidi ya dola milioni 400 kwa
ajili ya mwaka ujao, pia tumezungumza kuwa kutakuwa na dola milioni 800
zitakazotolewa na Marekani kwa ajili ya miradi mbalimbali na hii
haihusiani na MCC,” alisema Balozi Childress muda mfupi baada ya
kumaliza mazungumzo na Rais Magufuli.
“Ukweli ni kwamba tunayo mengi ya
kufanya pamoja katika sekta mbalimbali zikiwemo afya, elimu na kilimo na
tutafanya kila juhudi kuhakikisha haya yanafanikiwa,” alisema. Naye
Rais Magufuli alisema Serikali yake ya Awamu ya Tano, itaendeleza na
kuimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano na Marekani na kwamba fedha za
msaada kutoka Marekani ni muhimu kwa maendeleo ya Tanzania.
No comments:
Post a Comment
Comment here