KUTOKA BUNGENI:KANUNI ZA BUNGE ZALINDA POSHO ZA UPINZANI

UDHAIFU
wa Kanuni za Bunge katika kufafanua mambo mbalimbali ya uendeshaji wa
Bunge, umeelezwa na Naibu Spika, Dk Tulia Ackson kuwa unatakiwa
kurekebishwa ili kutoa nafasi ya Kiti cha Spika kutoa uamuzi dhidi ya
vitendo visivyokubalika vinavyoendelea ndani ya Bunge.Amesema
hayo jana alipokuwa akitoa majibu wa muongozo alioombwa na Waziri wa
Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe na Mbunge Nkasi Kaskazini, Ally
Keissy (CCM) kuhusu uhalali wa posho wanazolipwa wabunge wa Kambi ya
Upinzani, ambao wamekuwa wakiingia bungeni kusaini posho na kwenda
kupumzika.
Dk Tulia alisema tangu Mei 30, mwaka
huu, wabunge hao wamekuwa wakiingia bungeni kusaini posho na kuondoka
kwenda kupumzika, jambo lililosababisha Dk Mwakyembe kuomba muongozo
kama malipo hayo ni haki kwa mujibu wa masharti ya Ibara ya Katiba ya
23.
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Ibara ya 23, ibara ndogo ya kwanza na ya pili; “Kila mtu, bila
ya kuwapo ubaguzi wa aina yoyote, anayo haki ya kupata ujira
unaolingana na kazi yake, na watu wote wanaofanya kazi kulingana na
uwezo wao watapata malipo kulingana na kiasi na sifa za kazi
wanayoifanya.
Kila mtu anayefanya kazi anastahili
kupata malipo ya haki.” Akitoa muongozo wake kama malipo hayo ya posho
ni halali kwa mujibu wa Katiba au la, Naibu Spika alisema ametumia
uamuzi wa Kiti cha Spika uliotolewa Aprili 27, 2016 kuhusu muongozo kama
huo.
No comments:
Post a Comment
Comment here