Saturday, April 23, 2016

MR.BLUE: NGOMA YANGU NA ALI KIBA ITAACHA HISTORIA

Hitmaker wa baki na mimi ambaye hivi karibuni aliuaga ukapera kwa kuamua kufunga pingu za maisha na mzazi mwenzake Wayda, ameamua kuvunja ukimya na kuzungumzia kolabo yake na msanii nyota kwa sasa Alikiba aliyoipa jina la Mboga Saba.

Akizungumza na adamukihomile.com Mr. Blue amesema kuwa ngoma hiyo ipo tayari na anatarajia kuiachia wiki ijayo endapo mtayarishaji wa ngoma hiyo Man Water atamkabidhi, hivyo itakuwa rahisi kwake kuikabidhi kwa  mashabiki wake.

 ALIKIBA &MR BLUE

Blue ameongeza kuwa Mboga Saba ni ngoma ya aina yake ambayo anaimani itapokelewa vizuri na mashabiki wake kwa kuacha historia ya ngoma alizowahi kuzifanya, kwani wote wawili wameonesha umahiri mkubwa, katika hatua nyingine Blue amesema mashabiki wake wajiandae pia kwa ngoma mpya ya kundi lake la B.O.B Micharazo ambayo ameirekodi kwa Man Water.

 

No comments:

Post a Comment

Comment here