Saturday, April 23, 2016

MSHAMBULIAJI NYOTA EPL AKIRI KOSA HILI

Mshambuliaji wa vinara wa Ligi Kuu ya Uingereza Leicester City Jamie Vardy amekubali mashtaka ya utovu wa nidhamu.

Vardy mwenye umri wa miaka 29 alimkaripia mwamuzi Jon Moss baada ya kufukuzwa uwanjani kwa kadi nyekundu wakati wa mechi ya Jumapili ambayo walitoka sare 2-2 na West Ham.

Kwa kukubali shitaka hilo la Shirikisho la Soka la Uingereza (FA), Vardy, ambaye alikuwa ameitisha kikao cha kujitetea, huenda akaongezewa adhabu juu ya adhabu ya sasa ya kutoruhusiwa kucheza mchezo mmoja.

No comments:

Post a Comment

Comment here