PAPA WEMBA ALISHATABILI KIFO CHAKE
Papa Wemba mfalme wa muziki wa Lese Rumba almaarufu kama ‘Soukous’ alietamba miaka 1969 na Bendi maarufu ya ‘Soukous’ Zaiko
Langa Langa amekuwa Simba ambaye inaaminika ndiye mfalme wa mwituni kwa
kukamilisha mawindo yake kishujaa baada ya kufanikisha kile
alichotamani kitokee katika maisha yake ya Muziki wa Rumba nchini Kongo.
Amewahi
kunukuliwa na baadhi ya Vyombo vya Habari akisema kitu anachotamani
kitokee katika kukamilisha safari yake ya muziki hapa duniani ni kufia
stejini kwani ndio sehemu pekee ambayo hujihisi kama anapaa akiwa
anaimba.
“Nataka
nifie stejini, nataka siku zangu za mwisho ziwe jukwaani kwa sababu
kila muda ninapokuwa jukwaani nikiimba nahisi kama ninapaa”.
Ama kwa
hakika sisi sote viumbe wa Mungu na kwake tutarejea; alichokitabiri
Jules Shungu Wembadio Pene Kikumba almaarufu kama Papa Wemba kimetimia
Aprili 24 mwaka huu alipokuwa Abidjan nchini Ivory Coast
wakati akitumbuiza katika Tamasha la Festival des Musiques Urbaines
d’Anoumabo (FEMUA)
mwili wa Papa Wemba umewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kinshasa tayari kwa maziko .
No comments:
Post a Comment
Comment here