Sunday, June 19, 2016

JIFUNZE JINSI YA KUKOKOTOA GPA YAKO




wanachuo wa mount meru university-MMU



Karibu sana mpenzi msomaji wa blogu hii,Leo hii tutakuwa na somo jepesi sana kwa wanafunzi na wanachuo la kujifunza ni namna gani tunaweza kuzikokotoa GPA zetu  kupitia masomo tuyasomayo,haya sasa naomba tufuatane kuanzia mwanzo hadi mwisho ndugu yangu.
a)      Jambo la kwanza la kutambua ni kuelewa kila daraja linabeba pointi ngapi katika kutafuta GPA.
Daraja A pointi 5,B+ pointi 4,B pointi 3 na daraja C lina pointi 2.



b)      Unakumbuka zile hesabu za kutafuta wastani? Kama umesahau basi ni hivi,ukitaka wastani wa namba kadhaa mfano 1,2,3 na 4 huwa tunachukua jumla ya namba (1+2+3+4)=10 ambayo tunagawanya na idadi y namba ambazo zipo 4  hapa tukigawanya tutapata 2.5 (yaani 10 gawanya kwa 4)


c)       Sasa basi baada ya kujikumbusha hesabu hizi,cha kufanya ni wewe kujua idadi ya kozi zako huko SARMS zipo ngapi? Kwa mfano tufanye zipo 5


d)      Baada ya kujua madaraja ya kila kozi huko SARMS mf: kozi1 una A ,kozi2 una C,kozi 3 una B+,kozi 4 una B na kozi5 una A.
e)      Si unakumbuka pointi za  madaraja? Jikumbushe kipengele (a) hapo juu,umekumbuka eeeh! Jiulize una A ngapi katika kozi zako tano? Kwa mujibu wa matokeo una A mbili,basi fanya (2 mara 5=10),una B+ ngapi? Hapo inaonekana moja tu,basi fanya (1 mara 4=4),una B mbili (2 mara 3=6) na mwisho una C mija (1 mara 2=2).


f)       Sasa tunaanza kutafuta jumla ya pointi kwa tano,ambapo kwenye A kuna pointi 10,B+ kuna pointi 4,B kuna pointi 6 na C kuna pointi 2.
Jumla=10+4+6+2
            =22
Sasa hapa unaweza kupata GPA  yako kwa kuchukua jumla ya pointi ugawanye kwa idadi ya kozi ambazo ni tano tu
                                     =22/5
                                  GPA=4.4


            TEMBELEA KILA SIKU KWA HABARI MAKINI SANA

No comments:

Post a Comment

Comment here