MOUNT MERU UNIVERSITY OFFICIAL
MITIHANI YA
KUMALIZA MHULA WA PILI 2015/2016
(MOUNT MERU UNIVERSITY)
KUANZA
MAPEMA JUMATATU HII.
Wanafunzi wa Chuo kikuu cha mount meru
mkoani arusha,(leo) jumatatu wataaza mitihani yao ya kumaliza mhula wa pili.
Aidha mitihani hii itafanyika ndani ya wiki mbili (kuanzia tar
4/7/2016-18/7/2016) na baadae wanachuo hao kutawanyika katika maeneo mbalimbali ambako
watafanya mazoezi ya kile walichovuna kwa mwaka mzima. Mazoezi hayo maarufu
(TP) yatakuwa ni maalumu kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza na mwaka wa pili tofauti
na mwaka wa tatu ambao wakimaliza mtihani watalazimika kusubiri mpaka mwezi
oktoba ili kufanya mahafari.
bED ONE WALIA NA RATIBA YA
MTIHANI.
Kwa upande
mwingine ratiba imeonekana kuwa ni ngumu kwa wanafunzi wa BED ONE maana wiki ya
kwanza wana mtihani mmoja na wiki ya pili ikiwa mitihani minane.
Waziri wa
elimu alisema
“ratiba kama hii haiepukiki maana ofisi imezingatia sikukuu ya
IDD na sikukuu ya sabasaba na kalenda ya masomo kwa ujumla”.
Kwa upande
wake kiongozi wa BED ONE (CR), amevunja ukimya na kunena yafuatayo
“ratiba ni
ngumu ila ni ratiba rafiki kwa waliosoma”.
OFISI YAONYA.
Utawala
umetoa mwongozo kuwa madarasa yatayotumika ni HA4, HA5, HA6 NA HA7. Hivyo
mwanachuo anapashwa kufika muda mwafaka akiwa na kitambulisho na PASSBOOK na
aketi sehemu aliyopangwa.
Maonyo
mengine ambayo ofisi imetoa ni kama,
1. Kaa sehemu palipo na namba yako ya
usajili vinginevyo hutafanya mtihani.
2. Kama passbook yako haijasainiwa
katika ule ukurasa wa kijani, utatolewa nje ya mtihani.
3. Ukikamatwa na nyaraka zozote ambazo
huruhusiwi kuingia nazo kwenye chumba cha mtihani, utatolewa ndani ya chumba
cha mtihani na hautaruhusiwa kabisa kuendelea na mitihani.
4. Ukionekana umebadili ama kutoa namba
yako ya mtihani sehemu ilipo, hautaruhusiwa kuendelea na mitihani mingine.
Aidha ofisi
imesisitiza kila mhusika kuzingatia taarifa hizi.
UFAFANUZI KUHUSU MASUALA YA
FIELD
Waziri mwenye
kandarasi ya mikopo chuoni, amesema lipo tumaini kubwa la watu kupata pesa yao
ya FIELD kabla hawajaondoka. “Zoezi la upatikanaji wa pesa ya field liko hatua
za mwisho, watu watapewa pesa yao kabla hawaondoka na hata kama ikitokea
tumemaliza mitihani na bado pesa haipo, basi mimi nitakuwa wa mwisho kuondoka
hapa” alisema waziri.
Katika upande
mwingine kuna watu ambao majina yao hayakuonekana kwenye orodha ya wanafunzi
watakaofanya field sehemu mbalimbali kuanzia mapema mwezi august, Waziri wa
elimu amefuatilia , awali ilikuwa watu hao wangepangiwa kufanya field shule ya
MAGRETH , Lakini DVC AA ametoa mkono wa neema walau watu hao wafanye field
sehemu na shule yoyote ndani ya mkoa wa arusha. Siku ya ijumaa DVC AA atatoa
tena tamko la mwisho ambalo ndio litakuwa barikio la zoezi zima.
Dr west
No comments:
Post a Comment
Comment here