KAULI YA REAL MADRID BAADA YA KUFUNGIWA USAJILI WA MIAKA MIWILI
Alhamisi ya Januari 14 ilitoka taarifa
kutoka kwa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), kuwa limevifungia vilabu
vya Real Mdarid na Atletico Madrid kutokufanya usajili wowote mpaka
msimu wa 2017 na sababu ya kuvifungia ni kusajili wachezaji wenye umri
chini ya miaka 18 bila kufuata kanuni.
Aidha pamoja na adhabu hiyo ya
kutokusajili pia walipigwa faini na FIFA, Real Madrid ikitakiwa kulipa
pesa ya Uswisi, Francs 360,000 sawa na Pauni 250,000 na Atletico Madrid
ikipigwa faini ya Francs, 900,000 sawa na Pauni 620,000.
Baada ya FIFA kutoa taarifa hiyo, Real
Madrid kupitia kwa Mkurugenzi Mtendaji wa klabu hiyo, Jose Angel Sanchez
(pichani) ilisema kuwa adhabu hiyo siyo sahihi na haina uhakika na
wanaamini hata wakienda mahakamani watashinda.
Sanchez ambaye aliongozana na Mkuu wa
kitengo cha sheria wa Madrid, Javier Lopez Farre katika mkutano na
waandishi wa habari, alinukuliwa na gazeti la Marca kuwa adhabu
waliyopewa na FIFA siyo ya kuitarajia na haina ushahidi.
“Siyo
sahihi kwamba tulisajiri wachezaji chini ya miaka 18 bila kuwasajiri
RFEF (Chama cha Soka cha Hispania) na hiyo ndiyo sababu kuwa hatujafata
kanuni,
“Klabu
hii inafata sheria na watu ambao wanafanya kazi hapa hawajawahi kuvunja
sheria hizo, hoja ambayo wameitoa [FIFA] ina makosa,” alisema Sanchez.
Aidha baada ya kutoa taarifa hiyo, Real
Madrid wamepanga kwenda kukata rufaa kwenye mahakama sehemu ambayo
wanaamini watapata haki yao.
No comments:
Post a Comment
Comment here