WAKATI JK ALIYAFANYA HAYA KWA KUJIIBA,OBAMA HANA MUDA HUO,YEYE NI ‘KULA BATA’ KWENDA MBELE

WASHNGTON,Marekani
WAKATI wa utawala wa Rais wa awamu
ya nne Dr Jakaya Kikwete,moja kati ya jambo alilokuwa akililalamikia kwa
sana ni juu ya kukosa uhuru wa kufanya baadhi ya mambo yake binafsi kwa
kuwa alikuwa analindwa kila mara.
Dr
Kikwete alifikia hatua ya kusema kuwa anatamani amalize muda wake
haraka ili apate muda wa kufanya mambo yake bila ya kushirikisha
kurugenzi mbalimbali za uchunguzi na utafiti.
Moja
kati ya vitu alivyowahi kusema kuwa ‘anavimiss’ ni pamoja na kwenda
kucheza dansi pamoja na bao lakini pia alikuwa hawezi kula baadhi ya
vyakula kwa kile alichoelezwa kuwa vingeweza kumdhuru.
Hali
hii ilimfanya Dr Kikwete kufanya baadhi ya mambo kwa kujiiba ,mathalani
alijiiba kucheza mziki pindi anapokutana na wasanii ambapo hapo
angeweza kukata kiu yake ya kusakata rumba pamoja na wasanii bila ya
walinzi wake kumwingilia kwa kuwa hatua hiyo inakuwa miongoni mwa ratiba
zinazomtaka yeye kufanya hivyo.
Wakati
mwingine ambao aliutumia kujiiba toka katika mikono ya walinzi wake ni
wakati wa ziara mbalimbali za kitaifa na kimataifa,hapo Jk angeweza
kukutana na watu wake wa kitambo na kupiga nao soga muda mfupi kisha
kuendelea na ratiba nyingine.






Wakati mwingine pia Jk alitamani kulala
hata chini ili tu kukidhi haja yake ya kutaka uhuru wa kufanya kile
atakacho kama binadamu wa kawaida,ili kukidhi hayo pia alitumia fursa ya
ziara zake mbalimbali kutekeleza mambo kama hayo.
Lakini
hali hii ni tofauti kwa Rais wa Marekani,Barack Obama ambaye yeye
hufanya kila atakacho muda wowote ule ajisikiavyo bila kushurutishwana
walinzi wake.
Labda tu liwe jambo linaloweza kudhuru maisha yake,hapo angeweza kuongozwa kwanza kisha akaruhusiwa kufanya vile atakavyo.



Hivi hapa ni baadhi ya picha
zinazomwonyesha Obama akiwa kajiachia bila kuwepo hata mlinzi wake
karibu naye,wakati anakula kile akitakacho na kutmbea na watoto wake
katika safari zake za kifamilia
No comments:
Post a Comment
Comment here