WANAFUNZI CHUO CHA ST JOSEPH WATAKIWA KUSOMA HADI DIPLOMA
WANAFUNZI wa Chuo Kikuu cha St Joseph
(SJUIT) Kampasi ya Arusha (kilichofutiwa usajili), waliokuwa chini ya
programu ya shahada ya miaka mitano ya ualimu wa sayansi, wametakiwa
kusoma ngazi ya cheti au stashahada. Kama watataka kusoma ngazi ya juu,
watapaswa kuomba upya udahili.Aidha,
Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi imesema
wanafunzi waliokuwa wakipata mkopo kutoka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa
Elimu ya Juu (HESLB), mikopo yao pia imesimamishwa.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu,
Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Simon Msanjila alitoa
agizo hilo jana kupitia taaarifa kwa vyombo vya habari. Profesa Msanjila
alisema hatua hiyo, inatokana na kubainika kwamba wanafunzi hao
hawastahili kusoma shahada na pia hawakustahili kupewa mkopo.
“Tunawafahamisha wanafunzi wa SJUIT
waliokuwa kwenye programu ya miaka mitano kwamba watatakiwa kuishia
daraja la cheti na stashahada… Kama wanafunzi hao watataka kuendelea na
masomo ya juu, watatakiwa kuomba upya,” ilisema taarifa hiyo.
Februari 25, mwaka huu, Wizara kupitia
Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) baada ya kujiridhisha kuwa Kampasi ya Arusha ya
Chuo Kikuu cha Mt. Joseph Tanzania imepoteza sifa na vigezo vya
kuendelea kutoa elimu ya chuo kikuu, ilifuta kibali cha kuanzishwa
kwake.
No comments:
Post a Comment
Comment here